• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
TUNDUMA TOWN COUNCIL
TUNDUMA TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MJI TUNDUMA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mipango
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu
      • Divisheni ya Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Divisheni ya Miundombinu na Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Udhibiti Taka na Usafi wa Mazingira
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
  • Fursa na Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya , Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Lishe bora kwa Afya imara
      • Mapambano dhidi ya Malaria
      • Mapambano dhidi ya Dawa za Kulevya
      • Mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI
    • Huduma ya Elimu
      • Huduma ya Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Huduma ya Elimu ya Sekondari
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya Kilimo
    • Huduma ya Mifugo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Maendeleo ya Jamii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Uchumi, Mipango Takwimu
      • Kamati ya Elimu, Afya na maji
      • Kamati ya Kazi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Ethics Committee
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Instagram
    • Facebook
  • Nyaraka
    • Nyaraka
    • Miongozo

Majukwaa 15 ya Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi Yahuishwa Tunduma

Imewekwa : November 9th, 2023

Na Benton Nollo, Tunduma TC

Divisheni ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Mji Tunduma leo tarehe 09 Novemba 2023 imehitimisha rasmi zoezi la Uhuishaji wa Majukwaa ya Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi ambali limefanyika katika Kata zote 15 za Halmashauri hiyo.

Akizungumza katika Mkutano wa Wanawake Kata ya Majengo iliofanyika kwenye Ukumbi wa Soko la Machinga mjini Tunduma leo tarehe 09 Novemba 2023, Mratibu wa Dawati la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi wa Halmashauri ya Mji Tunduma, Edward Mbembela amesema lengo la Majukwaa hayo ni kuwakutanisha wanawake ili waweze kujadili fursa za kiuchumi na changamoto mbalimbali wanazokutana nazo wakati wa utekelezaji wsa shughuli za kiuchumi nchini.

Mbembela ametaja malengo mahsusi ya majukwaa hayo ni kuwakutanisha Wanawake wote katika ngazi zote za jamii ili kujadili fursa, changamoto na jinsi ya kushiriki katika shughuli za kiuchumi hususan biashara, kilimo, uchukuzi, usindikaji wa maliasili, ujenzi na madini.

“Majukwaa haya yatawasaidieni kuongeza uelewa kwenu kuhusu masuala ya uchumi, biashara, upatikanaji wa mitaji, sheria, ujasiriamali na matumizi ya teknolojia.” Amesema Mbembela na kuongeza;

“Ndugu zangu uwepo wa Majukwaa haya utasaidia kuhamasisha uanzishaji wa vikundi vya kiuchumi ili kunufaika na fursa za masoko na mikopo yenye masharti nafuu.”

Mbembela amesema pamoja na malengo hayo pia, Majukwaa hayo yatasaidia kupeana taarifa za fursa za kiuchumi na masoko miongoni mwa vikundi vya wanawake.

Mratibu huyo ameainisha kuwa zoezi hilo limefanyika kuanzia tarehe 01 hadi 09 Novemba 2023 ambapo Divisheni hiyo imefanikiwa kuhuisha majukwaa 15 ambapo wanawake 1,704 wameshiriki.

Kwa upande wake, Katibu wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi Halmashauri ya Mji Tunduma, Maua Sanga ameushukuru uongozi wa Halmashauri hiyo kupitia Divisheni ya Maendeleo ya Jamii kwa kuhakikisha Majukwaa yote 15 ya Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi yanahuishwa katika Kata zote kwa ufanisi mkubwa.

Aidha, Katibu huyo ametoa rai kwa wanawake wote kujitokeza kwa wingi katika vikao vya majukwaa vitakavyokuwa vikifanyika katika maeneo yao ili wasipitwe na fursa mbalimbali zinazoletwa na Wataalam wa Maendeleo ya Jamii.  


Matukio Katika Picha:


Matangazo

  • Tangazo la Mkutano wa Kawaida wa Baraza la Madiwani kwa Kipindi cha Robo ya Tatu ya Mwaka wa Fedha 2024/2025 May 14, 2025
  • Orodha ya Majimbo Mapya na Yaliyobadilishwa Majina May 12, 2025
  • Taarifa kwa Umma Kuhusu Watahiniwa 694 Kufanya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita 2025 May 03, 2025
  • Taarifa kwa Umma February 27, 2025
  • Onyesha Zote

Habari mpya

  • Mashindano ya UMISSETA Ngazi ya Halmashauri Yaanza Rasmi

    June 02, 2025
  • DAS Nkinda: Ziara ya Viongozi DR Congo Ina Manufaa Tunduma, Taifa

    May 30, 2025
  • Tunduma TC Yang'ara Mpira wa Miguu, Kwaya, Bongo Fleva UMITASHUMTA

    June 28, 2025
  • Dkt. Kasululu Ahitimisha Mashindano ya UMITASHUMTA

    May 28, 2025
  • Onyesha Zote

Maktaba ya video

Ubunifu mkoa wa Songwe
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Songwe Shindani Blogspot
  • Watumishi Portal
  • Tunduma yapata hati Inayoridhisha
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2019
  • Tangazo la kazi sekta ya Afya
  • Sherehe za Muungano
  • Kibali cha Matangazo

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti ya Mkoa wa Songwe
  • OR-TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Msampania, Chapwa - Tunduma

    Sanduku la Posta: P. O. BOX 73

    Simu ya Mezani: +255 25 2957388

    Simu ya Mkononi: +255 756 427 307

    Barua Pepe: td@tundumatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya mji Tunduma. Haki zote zimehifadhiwa