• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
TUNDUMA TOWN COUNCIL
TUNDUMA TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MJI TUNDUMA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mipango
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu
      • Divisheni ya Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Divisheni ya Miundombinu na Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Udhibiti Taka na Usafi wa Mazingira
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
  • Fursa na Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya , Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Lishe bora kwa Afya imara
      • Mapambano dhidi ya Malaria
      • Mapambano dhidi ya Dawa za Kulevya
      • Mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI
    • Huduma ya Elimu
      • Huduma ya Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Huduma ya Elimu ya Sekondari
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya Kilimo
    • Huduma ya Mifugo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Maendeleo ya Jamii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Uchumi, Mipango Takwimu
      • Kamati ya Elimu, Afya na maji
      • Kamati ya Kazi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Ethics Committee
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Instagram
    • Facebook
  • Nyaraka
    • Nyaraka
    • Miongozo

MGAO WA PIKIPIKI ZA MAMA SAMIA WAFIKA TUNDUMA

Imewekwa : February 21st, 2023

Afisa watendaji wa kata ya Chiwezi Halmashauri ya Mji Tunduma amekabidhiwa pikipiki iliyotolewa na serikali kwa lengo la kuboresha utendaji kazi na kurahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi nchini.

Hafla ya utoaji wa Pikipiki hiyo umefanyika leo tarehe 21/02/2023 katika ofisi za Halmasharui ya Mji Tunduma ambapo Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Ayubu Mlimba amemkabidhi Ndugu Paulo Jeremia Mwashiuya Afisa mtendaji kata ya chiwezi pikipki hiyo.

 
Mhe. Mlimba ameweka wazi kuwa kata ya Chiwezi ndio kata iliyo pembezoni zaidi mwa Mji wa Tunduma na inahusisha mitaa yenye wakulima na wafugaji ambao wanaishi umbali mrefu toka makao kamuu ya kata hivyo pikipiki hiyo ni kifaa muhimu kwa afisa huyo na inakwenda kumaliza changamoto ya kutembea umbali mrefu kuwafikia wanachi ili kutoa huduma.

Aidha amemtaka afisa mtendaji kuitumia pikipiki hiyo kwa ajili ya kazi iliyokusudiwa na serikali ya kuwahudumia wananchi na si vinginevyo huku akimsisitiza kuitunza na kuithamini kwa kutambua kuwa ni mali ya Umma.
"Tunamshukuru na Kumpongeza sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwathahamini Maafisa Watendaji wa kata, kwa kuwa wao ndio wanawahudumia wananchi moja kwa moja, tumepokea pikipiki moja ambayo leo hii tumemkabidhi mtendaji wa kata ya chiwezi ili ikachochee huduma na kusimamia miradi ya maendeleo” alisisitiza Mhe. Mlimba


Naye Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Tunduma ambaye ni Mkuu wa Divisheni ya Utumishi na Usimamizi wa Rasilimali watu Bwana Josephat Kayombo amesema kuwa nia ya serikali ni kurahisidha huduma kwa wananchi hivyo pikipiki hii itakuwa mkombozi mkubwa katika kuwahudumia wananchi kwa wakati na haraka zaidi tofauti na hapo zamani

“Pikipiki hii tumeitoa kwa kata ya chiwezi hivyo Mtendaji nakuomba uitunze na uhakikishe inafanya kazi za serikali kama malego ya Mhe. Rais, ikatokea unahama mtendaji atakayehamia katika kata hiyo basi aikute ikiwa nzuri na nzima ili iendelee kutoa huduma” alisema Bwana Kayombo

Pia kaimu mkurugenzi huyo aliendelea kumuelekeza Mtendaji kata kuhusu kuhakikisha matumizi sahihi ya pikipiki hiyo yanafuatwa

“Sitegemei kusikia pikipiki hii imekuwa ya kukodisha (bodaboda) hapo hatua za kinidhamu zitachukuliwa dhidi yako, nenda kaitumie katika kukurahishia kuwahudumia wananchi wa kata ya chiwezi na ninaimani kuwa sasa hata utendaji kazi utaongezeka zaidi” alisisitiza bwana kayombo

Kwa upandewake Afisa Mtendaji kata ya chiwezi Bwana Paulo Mwashiuya amemshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uamuzi wa kuwanunulia pikipiki watendaji wa kata kwani zitasaidia sana kuwafikia wananchi haraka na kuweza kutatua kero zinazowakumba kwa muda muafaka

“Ninaahidi kuwa pikipiki hii nitaitumia katika majumu yangu ya kila siku ya Utendaji wa kata na hasa katika kuwatumikia wananchi wa kata ya chiwezi, sitoweza kuitumia katika masuala ambayo ni kinyume na matakwa ya ajira yangu na kazi zangu” alisema Mtendaji Mwashiuya

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilinunua Pikipiki 916 ambazo zilikabidhiwa kwa Watendaji wa Kata na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango, kwenye ukumbi wa Jiji la Dodoma uliopo Mtumba tarehe 14/02/2022


Matangazo

  • Tangazo la Mkutano wa Kawaida wa Baraza la Madiwani kwa Kipindi cha Robo ya Tatu ya Mwaka wa Fedha 2024/2025 May 14, 2025
  • Orodha ya Majimbo Mapya na Yaliyobadilishwa Majina May 12, 2025
  • Taarifa kwa Umma Kuhusu Watahiniwa 694 Kufanya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita 2025 May 03, 2025
  • Taarifa kwa Umma February 27, 2025
  • Onyesha Zote

Habari mpya

  • Mashindano ya UMISSETA Ngazi ya Halmashauri Yaanza Rasmi

    June 02, 2025
  • DAS Nkinda: Ziara ya Viongozi DR Congo Ina Manufaa Tunduma, Taifa

    May 30, 2025
  • Tunduma TC Yang'ara Mpira wa Miguu, Kwaya, Bongo Fleva UMITASHUMTA

    June 28, 2025
  • Dkt. Kasululu Ahitimisha Mashindano ya UMITASHUMTA

    May 28, 2025
  • Onyesha Zote

Maktaba ya video

Ubunifu mkoa wa Songwe
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Songwe Shindani Blogspot
  • Watumishi Portal
  • Tunduma yapata hati Inayoridhisha
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2019
  • Tangazo la kazi sekta ya Afya
  • Sherehe za Muungano
  • Kibali cha Matangazo

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti ya Mkoa wa Songwe
  • OR-TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Msampania, Chapwa - Tunduma

    Sanduku la Posta: P. O. BOX 73

    Simu ya Mezani: +255 25 2957388

    Simu ya Mkononi: +255 756 427 307

    Barua Pepe: td@tundumatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya mji Tunduma. Haki zote zimehifadhiwa