• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
TUNDUMA TOWN COUNCIL
TUNDUMA TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MJI TUNDUMA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mipango
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu
      • Divisheni ya Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Divisheni ya Miundombinu na Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Udhibiti Taka na Usafi wa Mazingira
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
  • Fursa na Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya , Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Lishe bora kwa Afya imara
      • Mapambano dhidi ya Malaria
      • Mapambano dhidi ya Dawa za Kulevya
      • Mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI
    • Huduma ya Elimu
      • Huduma ya Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Huduma ya Elimu ya Sekondari
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya Kilimo
    • Huduma ya Mifugo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Maendeleo ya Jamii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Uchumi, Mipango Takwimu
      • Kamati ya Elimu, Afya na maji
      • Kamati ya Kazi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Ethics Committee
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Instagram
    • Facebook
  • Nyaraka
    • Nyaraka
    • Miongozo

SHULE ZOTE ZA UMMA TANZANIA KUENDESHWA KIDIGITALI

Imewekwa : November 6th, 2022

Serikali imezindua zoezi la ugawaji vishikwambi kwa walimu nchini na kuzitaka Mamlaka zinazohusika na kazi hiyo kuhakikisha vishikwambi hivyo vinawafikia walengwa ili viweze kufanya kazi iliyokusudiwa.

Akizungumza Jijini Dodoma wakati wa uzinduzi huo Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amesema vishikwambi hivyo vinalenga kuboresha mchakato wa utoaji elimu ili kuinua ubora wa elimu nchini, hivyo ni vizuri vikawafikia walengwa ili lengo liweze kutimia.

“Hapa ningependa kusisitiza kuwa vishikwambi hivi ni kwa ajili ya walimu tu na si vinginevyo hivyo Viongozi wote wa Serikali mliopo OR- TAMISEMI, Halmashauri na wale wote watakaokuwa na jukumu la kugawa vishikwambi hivi hakikisheni hakuna mwalimu atakayekosa,” amesisitiza Mhe. Majaliwa.

Amesema Serikali ya Awamu ya Sita tangu kuingia madarakani imewekeza kwa kiasi kikubwa kwenye TEHAMA ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya Mwaka 2020 - 2025 ambayo inasisitiza matumizi ya TEHAMA katika ngazi mbalimbali za Elimu ili kuchochea ukuaji wa uchumi na kuboresha maisha ya watu kwa ujumla.

“Walimu hakikisheni mnatumia vishikwambi hivi katika kuboresha mchakato wa utoaji elimu ili kuinua ubora wa elimu nchini na si vinginevyo na naamini mtahamasika katika kutumia TEHAMA katika ufundishaji na ujifunzaji,” ameongeza Mhe. Majaliwa.

Kwa upande wake Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema Wizara ya Elimu imenunua jumla ya Vishikwambi 300,000 kwa lengo la kuendelea kuboresha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji nchini.

Amesema vishikwambi hivyo vinakwenda kurahisisha upatikanaji wa nyenzo za kufundishia na kujifunzia, kuongeza idadi ya walimu watakaotumia mfumo wa kujifunzia wa Taasisi ya Elimu Tanzania unaojulikana kwa jina la Learning Management System (LMS) na kuhama kutoka mfumo wa usahihishaji wa mitihani wa makaratasi kwenda mfumo wa usahihishaji wa mitihani kwa njia ya mtandao - (e-marking system).







Matangazo

  • Taarifa kwa Umma Kuhusu Watahiniwa 694 Kufanya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita 2025 May 03, 2025
  • Taarifa kwa Umma February 27, 2025
  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili January 24, 2025
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2024 January 23, 2025
  • Onyesha Zote

Habari mpya

  • Waziri Aweso Aagiza Mradi wa Maji Tunduma, Vwawa Kukamilika kwa Wakati

    March 20, 2025
  • 'Ahadi Imetimia, Bilioni 119.9 Kutumika Mradi wa Maji Tunduma, Vwawa'

    May 20, 2025
  • Wananchi Wanatarajia Uongozi Bora Kutoka Kwenu: DC Mwandobo

    March 05, 2025
  • Tusisahau Tulikotoka: TD Chaurembo

    March 05, 2025
  • Onyesha Zote

Maktaba ya video

Ubunifu mkoa wa Songwe
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Songwe Shindani Blogspot
  • Watumishi Portal
  • Tunduma yapata hati Inayoridhisha
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2019
  • Tangazo la kazi sekta ya Afya
  • Sherehe za Muungano
  • Kibali cha Matangazo

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti ya Mkoa wa Songwe
  • OR-TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Msampania, Chapwa - Tunduma

    Sanduku la Posta: P. O. BOX 73

    Simu ya Mezani: +255 25 2957388

    Simu ya Mkononi: +255 756 427 307

    Barua Pepe: td@tundumatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya mji Tunduma. Haki zote zimehifadhiwa