• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
TUNDUMA TOWN COUNCIL
TUNDUMA TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MJI TUNDUMA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mipango
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu
      • Divisheni ya Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Divisheni ya Miundombinu na Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Udhibiti Taka na Usafi wa Mazingira
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
  • Fursa na Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya , Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Lishe bora kwa Afya imara
      • Mapambano dhidi ya Malaria
      • Mapambano dhidi ya Dawa za Kulevya
      • Mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI
    • Huduma ya Elimu
      • Huduma ya Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Huduma ya Elimu ya Sekondari
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya Kilimo
    • Huduma ya Mifugo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Maendeleo ya Jamii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Uchumi, Mipango Takwimu
      • Kamati ya Elimu, Afya na maji
      • Kamati ya Kazi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Ethics Committee
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Instagram
    • Facebook
  • Nyaraka
    • Nyaraka
    • Miongozo

TUNDUMA YAONGOZA TENA MITIHANI KIDATO CHA SITA 2022

Imewekwa : July 5th, 2022

Halmashauri ya Mji Tunduma imeendelea kufanya vizuri katika mitihani ya kidato cha sita

Shule ya Mwalimu J. K. Nyerere imeendelea kufanya vizuri na kuongeza ufaulu kila mwaka ambapo mwaka 2022 shule hii ilikuwa na watahiniwa 100 kwa Tahasusi mbalimbali, shule hii imefanikiwa kushika nafasi ya 4 Kimkoa na kufaulisha wanafunzi wote walio fanya mtihani wa kidato cha sita

Katika ufaulu wake Shule ya Mwalimu J. K. Nyerere imefanikiwa kufaulisha kama ifuatavyo:-

 Daraja la      I – 30

Daraja la       II – 57

Daraja            III – 13

Daraja            IV – 0 

Daraja la       0 – 0

kwa upande wa shule ya Wasichana ya Mpemba Sekondari nayo imeibuka kidedea kwa kufaulisha wanafunzi wote kwani walikuwa watahiniwa 62 na imeshika nafasi ya 6 kimkoa na kuzibwaga shule kongwe nyingi mkoani songwe

Katika ufaulu wake Shule ya Sekondari Mpemba imefanikiwa kufaulisha kama ifuatavyo:-

 Daraja la      I – 14

Daraja la       II – 44

Daraja            III – 4

Daraja            IV – 0 

Daraja la       0 – 0

Matokeo hayo yametangazwa leo na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) ambapo watahiniwa wote 162 waliofanya mtihani kwa shule mbili za Halmashauri ya Mji Tunduma wamefaulu.

Ufaulu huu ni kutokana na Jitihada za Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Tunduma Mhe. Ayubu Mlimba, Mkurugenzi wa Halmamashauri ya Mji Tunduma Bwana Philemon Magesa, walimu wa Shule zote, watumishi, madiwani pamoja na Wazazi wa wanafunzi hao

Akiongea kwa njia ya Simu Mwenyekiti wa Halimashauri ya Mji Tunduma (Diwani wa kata ya mwakakati) Mhe. Ayubu Mlimba amefurahi sana na kusema kuwa

“Motisha tuliyoitoa inafanya kazi, kama Halmashauri ya Mji Tunduma tunatoa Tsh. 10,000/= kwa kila alama A ya somo lolote katika mitihani ya Taifa na kufanya hali ya waalimu kujituma, sasa matunda yake ndio haya yanaonekana” alisema Mhe. Mlimba

Pia Mhe. Mlimba alisema kuwa mshikamano na umoja wa watumishi wa Halmashauri pamoja na uongozi madhubuti wa Afisa elimu sekondari aliye chini ya Mkurugenzi ni chachu ya mafanikio haya

Naye Mkurugenzi wa Halimashauri ya Mji Tunduma Bwana Philemon Magesa amewapongeza sana walimu na wanafunzi hao kwa matokeo mazuri waliyoyapata kwani yanaifanya Tunduma ing’ae katika Nyanja ya Elimu.

 

Mkurugenzi Magesa pia alisema kuwa ufaulu huu pia unachangiwa na ujenzi wa miundombinu ambayo inajengwa katika kuhakikisha wanafunzi wa walimu wanapata madarasa na ofisi bora ili kukidhi haja ya kusoma kwa weledi

“Tunamshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia pesa za UVIKO – 19 za kujengea madarasa na kununua madawati, jambo hilo limepunguza sana msongamano kwa wanafunzi darasani na kuongeza ufaulu” alisema Bwana Magesa

 Kwa upande wake Afisa Elimu Sekondari Bi. Patricia Mbigili amewapongeza sana walimu kwa kushirikiana katika malezi na usimamizi wa masomo kwa wanafunzi wote na kuwataka waendeleze mbinu hizo kwa wanafunzi wengine waliobaki ili Tunduma ije ishike nafasi ya juu kitaifa.

“Kazi yangu kama Afisa Elimu ni kuwaongoza walimu katika kutoa elimu bora kwa wanafunzi pamoja na malezi, kwa hiyo ufaulu wa wanafuzi wote 162 ni kiashiria kwamba maelekezo na maoini yangu yanazingatiwa ndio maana leo hii tumefika hapa” alisema Bi. Mbigili

Matangazo

  • Tangazo la Mkutano wa Kawaida wa Baraza la Madiwani kwa Kipindi cha Robo ya Tatu ya Mwaka wa Fedha 2024/2025 May 14, 2025
  • Orodha ya Majimbo Mapya na Yaliyobadilishwa Majina May 12, 2025
  • Taarifa kwa Umma Kuhusu Watahiniwa 694 Kufanya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita 2025 May 03, 2025
  • Taarifa kwa Umma February 27, 2025
  • Onyesha Zote

Habari mpya

  • Mashindano ya UMISSETA Ngazi ya Halmashauri Yaanza Rasmi

    June 02, 2025
  • DAS Nkinda: Ziara ya Viongozi DR Congo Ina Manufaa Tunduma, Taifa

    May 30, 2025
  • Tunduma TC Yang'ara Mpira wa Miguu, Kwaya, Bongo Fleva UMITASHUMTA

    June 28, 2025
  • Dkt. Kasululu Ahitimisha Mashindano ya UMITASHUMTA

    May 28, 2025
  • Onyesha Zote

Maktaba ya video

Ubunifu mkoa wa Songwe
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Songwe Shindani Blogspot
  • Watumishi Portal
  • Tunduma yapata hati Inayoridhisha
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2019
  • Tangazo la kazi sekta ya Afya
  • Sherehe za Muungano
  • Kibali cha Matangazo

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti ya Mkoa wa Songwe
  • OR-TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Msampania, Chapwa - Tunduma

    Sanduku la Posta: P. O. BOX 73

    Simu ya Mezani: +255 25 2957388

    Simu ya Mkononi: +255 756 427 307

    Barua Pepe: td@tundumatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya mji Tunduma. Haki zote zimehifadhiwa