• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
TUNDUMA TOWN COUNCIL
TUNDUMA TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MJI TUNDUMA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mipango
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miipangofiji na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwaimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Fursa na Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Uchumi, Mipango Takwimu
      • Kamati ya Elimu, Afya na maji
      • Kamati ya Kazi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Ethics Committee
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

TUNDUMA YAONGOZA TENA MITIHANI KIDATO CHA SITA 2022

Imewekwa : July 5th, 2022

Halmashauri ya Mji Tunduma imeendelea kufanya vizuri katika mitihani ya kidato cha sita

Shule ya Mwalimu J. K. Nyerere imeendelea kufanya vizuri na kuongeza ufaulu kila mwaka ambapo mwaka 2022 shule hii ilikuwa na watahiniwa 100 kwa Tahasusi mbalimbali, shule hii imefanikiwa kushika nafasi ya 4 Kimkoa na kufaulisha wanafunzi wote walio fanya mtihani wa kidato cha sita

Katika ufaulu wake Shule ya Mwalimu J. K. Nyerere imefanikiwa kufaulisha kama ifuatavyo:-

 Daraja la      I – 30

Daraja la       II – 57

Daraja            III – 13

Daraja            IV – 0 

Daraja la       0 – 0

kwa upande wa shule ya Wasichana ya Mpemba Sekondari nayo imeibuka kidedea kwa kufaulisha wanafunzi wote kwani walikuwa watahiniwa 62 na imeshika nafasi ya 6 kimkoa na kuzibwaga shule kongwe nyingi mkoani songwe

Katika ufaulu wake Shule ya Sekondari Mpemba imefanikiwa kufaulisha kama ifuatavyo:-

 Daraja la      I – 14

Daraja la       II – 44

Daraja            III – 4

Daraja            IV – 0 

Daraja la       0 – 0

Matokeo hayo yametangazwa leo na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) ambapo watahiniwa wote 162 waliofanya mtihani kwa shule mbili za Halmashauri ya Mji Tunduma wamefaulu.

Ufaulu huu ni kutokana na Jitihada za Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Tunduma Mhe. Ayubu Mlimba, Mkurugenzi wa Halmamashauri ya Mji Tunduma Bwana Philemon Magesa, walimu wa Shule zote, watumishi, madiwani pamoja na Wazazi wa wanafunzi hao

Akiongea kwa njia ya Simu Mwenyekiti wa Halimashauri ya Mji Tunduma (Diwani wa kata ya mwakakati) Mhe. Ayubu Mlimba amefurahi sana na kusema kuwa

“Motisha tuliyoitoa inafanya kazi, kama Halmashauri ya Mji Tunduma tunatoa Tsh. 10,000/= kwa kila alama A ya somo lolote katika mitihani ya Taifa na kufanya hali ya waalimu kujituma, sasa matunda yake ndio haya yanaonekana” alisema Mhe. Mlimba

Pia Mhe. Mlimba alisema kuwa mshikamano na umoja wa watumishi wa Halmashauri pamoja na uongozi madhubuti wa Afisa elimu sekondari aliye chini ya Mkurugenzi ni chachu ya mafanikio haya

Naye Mkurugenzi wa Halimashauri ya Mji Tunduma Bwana Philemon Magesa amewapongeza sana walimu na wanafunzi hao kwa matokeo mazuri waliyoyapata kwani yanaifanya Tunduma ing’ae katika Nyanja ya Elimu.

 

Mkurugenzi Magesa pia alisema kuwa ufaulu huu pia unachangiwa na ujenzi wa miundombinu ambayo inajengwa katika kuhakikisha wanafunzi wa walimu wanapata madarasa na ofisi bora ili kukidhi haja ya kusoma kwa weledi

“Tunamshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia pesa za UVIKO – 19 za kujengea madarasa na kununua madawati, jambo hilo limepunguza sana msongamano kwa wanafunzi darasani na kuongeza ufaulu” alisema Bwana Magesa

 Kwa upande wake Afisa Elimu Sekondari Bi. Patricia Mbigili amewapongeza sana walimu kwa kushirikiana katika malezi na usimamizi wa masomo kwa wanafunzi wote na kuwataka waendeleze mbinu hizo kwa wanafunzi wengine waliobaki ili Tunduma ije ishike nafasi ya juu kitaifa.

“Kazi yangu kama Afisa Elimu ni kuwaongoza walimu katika kutoa elimu bora kwa wanafunzi pamoja na malezi, kwa hiyo ufaulu wa wanafuzi wote 162 ni kiashiria kwamba maelekezo na maoini yangu yanazingatiwa ndio maana leo hii tumefika hapa” alisema Bi. Mbigili

Matangazo

  • MAJINA YA WALIOPITA KATIKA USAILI WA ZOEZI LA SENSA 2022 HALMASHAURI YA MJI TUNDUMA July 28, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WASIMAMIZI WA TEHAMA KATIKA ZOEZI LA SENSA 2022 July 18, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WASIMAMIZI WA MAUDHUI KATIKA ZOEZI LA SENSA 2022 July 19, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI MAKARANI KATIKA ZOEZI LA SENSA 2022 July 19, 2022
  • Onyesha Zote

Habari mpya

  • TUNDUMA YAONGOZA TENA MITIHANI KIDATO CHA SITA 2022

    July 05, 2022
  • SHEREHE ZA UTIAJI SAINI KATI YA TBA NA TUNDUMA ZAFANYIKA

    June 27, 2022
  • TUNDUMA KINARA HOJA ZA CAG MKOA WA SONGWE YAPATA HATI INAYORIDHISHA MIAKA SITA MFULULIZO

    June 24, 2022
  • NMB TUNDUMA YAFUNGA MWAKA KIVINGINE

    June 20, 2022
  • Onyesha Zote

Maktaba ya video

Ubunifu mkoa wa Songwe
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Songwe Shindani Blogspot
  • Watumishi Portal
  • Tunduma yapata hati Inayoridhisha
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2019
  • Tangazo la kazi sekta ya Afya
  • Sherehe za Muungano
  • Kibali cha Matangazo

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya Serikali

Idadi ya watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Msampania, Chapwa - Tunduma

    Sanduku la Posta: P. O. BOX 73

    Simu ya Mezani: +255 25 2957388

    Simu ya Mkononi: +255 752 807 767

    Barua Pepe: td@tundumatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya mji Tunduma. Haki zote zimehifadhiwa