• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
TUNDUMA TOWN COUNCIL
TUNDUMA TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MJI TUNDUMA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mipango
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miipangofiji na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwaimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Fursa na Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Uchumi, Mipango Takwimu
      • Kamati ya Elimu, Afya na maji
      • Kamati ya Kazi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Ethics Committee
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

ZIARA YA KATIBU MKUU YALETA NEEMA TUNDUMA

Imewekwa : June 3rd, 2022

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Ndugu Tikson Nzunda leo tarehe 01/06/2022 amefanya ziara ya siku Moja ndani ya Halmashauri ya MjiTunduma.


Akiongea na wakuu wa Divisheni na Vitengo wa Halmashauri ya Mji Tunduma, Amesema kuwa Tanzania kwa sasa inatakiwa kufuga kisasa ili matokeo yaonekane na sio kufuga kienyeji kama zamani

 Katibu Mkuu Nzunda pia amesema Wizara imeamua kufufua vyuo vyote vilivyokuwa havifanyi kazi kwa weledi na kuamua kupeleka vijana ili wakajifunze stadi mbalimbali uzalishaji wa mifugo wenye tija.


Katika maelezo yake ndugu Nzunda alisema kwa sasa wafugaji wanatakiwa kutumia eneo dogo la uzalishaji (Zero Grazing) kwa kuwa na malisho bora na kuwepo kwa mashamba darasa ya mfano ya malisho kwa wafugaji walau hata kwa hekari moja kila kata za kimkakati ili waweze kujifunza mbinu za uzajilshaji wa malisho bora kwa chakula cha mifugo ili kuongeza uzalishaji wa Maziwa

Pia Katibu mkuu alisisitiza kuwepo mkakati wa kichimba visima vya maji na mabwawa kwa kata za kimkakati ili kuweza kuwasaida wafugaji katika kuhudumia mifugo kwa kunywesha maji safi na salama kwa mifugo yao


“Afya za mifugo zishughulikiwe kwa kudhibiti magonjwa ya Mlipuko na yasiyo ya mlipuko kwa kufanya chanjo ya mifugo ambayo inatakiwa itolewe kwa ratiba moja kwa pamoja ili Halmashauri nzima iweze kuchanja mifugo yote na kuondokana na baadhi ya mifugo kubaki na magonjwa ambayo yanaweza kusababisha magonjwa kwa mifugo mingine. Chango ya Mifugo ni Lazima na sio hiyari hivyo kila mfugaji analazimika mara ratiba ikitoka kupeleka mifugo yake kwenye Chanjo husika” alisema Nzunda

Pia katika kudhibili majongwa yatokanayo na vimelea vya kupe ni lazima kila Mfugajio aogeshe mifugo yake kwa kupeleka kwenye majosho na kama Josho halipo basi watumie Bomba la mkono kuogesha mifugo yao


Pia alishauri Kuanzishwa kwa mnada mkubwa wa mifugo na mazao ya mifugo ambao unaweza kutumika katika kuuza bidhaa ndani na nje ya nchi ukizingatia Tunduma ipo Mpakani mwa nchi za SADC


Pia alisisitiza kuwa Mifugo haitakiwi kuchungwa au kuswagwa katika barabara kwani sio tu inaharibu miundombinu ya barabara bali inakosa ubora wa afya zao, kwani imekuwa ikitembea umbali mrefu sana mfano kutoka mkoa mmoja hadi mwingine na kufanya kupata majonjwa au kuambukiza mifugo mingine katika eneo ambalo halikuwa na magonjwa


Katibu mkuu alimshukuru Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Tunduma kwa kuwawezesha vitendea kazi maafisa Ugani katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku hata hivyo jitihada za kuendelea kuwezesha Divisheni za uzalishaji ili ziendelee kuwa na ari ya kufanya kazi


Katika kuhitimisha Katibu mkuu alimpongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Tunduma kwa kuweza kukusanya mapato ya Ndani kwa Zaidi ya asilimia miamoja. Kwani  Halmashauri ya Mji Tunduma ilipanga kukusanya Tzs 7,600,000,000/= kwa bajeti ya mwaka wa fedha 2021/2022. Hata hivyo Halmashauri ya Mji Tunduma mpaka Mei 31/2022 imeweza kukusanya kiasi cha Tzs 7,635,690,500/= ambayo sawa na 100.8%

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA May 24, 2022
  • TAARIFA KWA UMMA July 25, 2021
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA TUNDUMA May 03, 2022
  • KUITWA KAZINI June 25, 2021
  • Onyesha Zote

Habari mpya

  • TUNDUMA KINARA HOJA ZA CAG MKOA WA SONGWE YAPATA HATI INAYORIDHISHA MIAKA SITA MFULULIZO

    June 24, 2022
  • NMB TUNDUMA YAFUNGA MWAKA KIVINGINE

    June 20, 2022
  • NIMEFURAHISHWA SANA MAPOKEZI YA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO TUNDUMA

    June 22, 2022
  • KILA MTUMISHI AHAKIKISHE ANAFUNGA MWAKA AKIWA AMEMALIZA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAKE_TD MAGESA

    June 17, 2022
  • Onyesha Zote

Maktaba ya video

Ubunifu mkoa wa Songwe
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Songwe Shindani Blogspot
  • Watumishi Portal
  • Tunduma yapata hati Inayoridhisha
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2019
  • Tangazo la kazi sekta ya Afya
  • Sherehe za Muungano
  • Kibali cha Matangazo

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya Serikali

Idadi ya watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Msampania, Chapwa - Tunduma

    Sanduku la Posta: P. O. BOX 73

    Simu ya Mezani: +255 25 2957388

    Simu ya Mkononi: +255 752 807 767

    Barua Pepe: td@tundumatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya mji Tunduma. Haki zote zimehifadhiwa