• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
TUNDUMA TOWN COUNCIL
TUNDUMA TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MJI TUNDUMA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mipango
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu
      • Divisheni ya Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Divisheni ya Miundombinu na Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Udhibiti Taka na Usafi wa Mazingira
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
  • Fursa na Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya , Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Lishe bora kwa Afya imara
      • Mapambano dhidi ya Malaria
      • Mapambano dhidi ya Dawa za Kulevya
      • Mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI
    • Huduma ya Elimu
      • Huduma ya Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Huduma ya Elimu ya Sekondari
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya Kilimo
    • Huduma ya Mifugo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Maendeleo ya Jamii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Uchumi, Mipango Takwimu
      • Kamati ya Elimu, Afya na maji
      • Kamati ya Kazi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Ethics Committee
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Instagram
    • Facebook
  • Nyaraka
    • Nyaraka
    • Miongozo

HAMKUWA WAFANYAKAZI TU BALI NDUGU ZANGU KWAHERINI WANA SONGWE _ RC KINDAMBA

Imewekwa : March 21st, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Waziri Kindamba amesema kuwa hajutii kufanya kazi katika mkoa wa Songwe kutokana na ushirikiano alioupata kutaka kwa watumishi wa umma na wananchi wakati akiwa mkuu wa mkoa huo huku akiahidi kuwa Songwe itaendelea kubaki moyoni mwake.


Kindamba alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Songwe akihamishiwa mkoa wa Tanga na Rais Samia Suluhu Hassan Februari 26 mwaka huu ambapo nafasi yake ikichukuliwa na Dkt Francis Michael.


Akizungumza wakati wa kukabidhiana ofisi na mkuu wa mkoa huo mpya leo Jumatatu Machi 20, 2023 Kindamba amesema wafanyakazi wengi katika mkoa huo waliishi naye kama ndugu hivyo Songwe itaendelea kubaki moyoni mwake.


"Hamkuwa wafanyakazi tu ila mlikuwa ndugu zangu, mara nyingi familia yangu ilikuwa Dar es Salaam lakini ninyi mlikuwa kama ndugu zangu, kutokana na ushirikiano mliokuwa mnanipa. Sijawahi kujutia kufanya kazi Songwe na itaendelea kubaki moyoni mwangu" amewaambia viongozi na watumishi wa mkoa huo wakati akikabidhi ofisi.


Amebainisha kuwa uahirikiano alioupata ndio uliowezesha kutatua mogogoro ya mara kwa mara katika mji wa Tunduma.


"Tunduma ilikuwa inachemka na migogoro lakini tuliweza kushirikishana na kwa ushirikiano mambo yakawa shwari. Tunduma imepoa kwa sababu ya kushirikishana kutatua migogoro" amesema Kindamba na kuongeza


"Nawashukuru viongozi wenzangu kuanzia ngazi ya mkoa hadi vijiji, tulifanikiwa kwa sababu tulifanya kazi kama timu"


Pia, Kindamba amewataka viongozi na wananchi wa mkoa wa Songwe kupinga ukatili wa kijinsia na vitendo vingine vinavyokwenda kinyume na maadili.


Hata hivyo, Kindamba amemshauri mkuu wa mkoa huyo kuendeleza vipaumbele vilivyokuwa vimewekwa ikiwemo ujenzi wa Bandari Kavu eneo la Mpemba, upanuzi wa barabara ya TANZAM iwe njia nne, mji wa kisasa kata ya Mpemba, stendi ya kisasa ya mkoa na utatuzi wa migogoro ya mipaka.


Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Songwe (RAS), Bi. Happiness Seneda amemshukuru Kindamba kwa namna alivyoishi vizuri na watumishi wa umma wa mkoa huo na kubainisha kuwa Mkuu huyo wa mkoa wa Tanga alikuwa mwalimu kwa wengi wakati akiwa katika mkoa huo.

Matangazo

  • Tangazo la Mkutano wa Kawaida wa Baraza la Madiwani kwa Kipindi cha Robo ya Tatu ya Mwaka wa Fedha 2024/2025 May 14, 2025
  • Orodha ya Majimbo Mapya na Yaliyobadilishwa Majina May 12, 2025
  • Taarifa kwa Umma Kuhusu Watahiniwa 694 Kufanya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita 2025 May 03, 2025
  • Taarifa kwa Umma February 27, 2025
  • Onyesha Zote

Habari mpya

  • Mashindano ya UMISSETA Ngazi ya Halmashauri Yaanza Rasmi

    June 02, 2025
  • DAS Nkinda: Ziara ya Viongozi DR Congo Ina Manufaa Tunduma, Taifa

    May 30, 2025
  • Tunduma TC Yang'ara Mpira wa Miguu, Kwaya, Bongo Fleva UMITASHUMTA

    June 28, 2025
  • Dkt. Kasululu Ahitimisha Mashindano ya UMITASHUMTA

    May 28, 2025
  • Onyesha Zote

Maktaba ya video

Ubunifu mkoa wa Songwe
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Songwe Shindani Blogspot
  • Watumishi Portal
  • Tunduma yapata hati Inayoridhisha
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2019
  • Tangazo la kazi sekta ya Afya
  • Sherehe za Muungano
  • Kibali cha Matangazo

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti ya Mkoa wa Songwe
  • OR-TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Msampania, Chapwa - Tunduma

    Sanduku la Posta: P. O. BOX 73

    Simu ya Mezani: +255 25 2957388

    Simu ya Mkononi: +255 756 427 307

    Barua Pepe: td@tundumatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya mji Tunduma. Haki zote zimehifadhiwa