• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
TUNDUMA TOWN COUNCIL
TUNDUMA TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MJI TUNDUMA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mipango
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miipangofiji na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwaimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Fursa na Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Uchumi, Mipango Takwimu
      • Kamati ya Elimu, Afya na maji
      • Kamati ya Kazi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Ethics Committee
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

KIKAO CHA MAANDALIZI YA SENSA

Imewekwa : June 15th, 2022


Halmashauri ya Mji Tunduma imeanza vikao vya kujiandaa kwa ajili ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 kwa watendaji wa Kata na mitaa yote ya Halmashauri ya Mji Tunduma

Akiongea katika kikao kazi hicho Mratibu wa Sensa ya watu na makazi wa Halmashauri ya Mji Tunduma Bi. Angela Francis Njaritta amewaeleza watendaji wa kata na mitaa juu ya umuhimu mkubwa wa Sensa na Faida zake

 Katika wasilisho lake Bi. Angela aliwaambia washiriki kuwa “Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 kama zilivyo sensa nyingine zilizotangulia itatoa majawabu katika mambo ya msingi yanayohusu watu kiafya, kielimu, kijamii, kimazingira na kiuchumi”

Upimaji wa mipango mbalimbali ya Serikali hutegemea taarifa zinazotokana aidha na Sensa au Tafiti ambazo chimbuko lake ni Sensa ya Watu na Makazi

Pia Bi. Angela alieleza Sababu za kufanya sense katika nchi ni;

Kwanza ni kwa mujibu wa Sheria ya Takwimu SURA 351 ambayo inamuagiza Mtakwimu Mkuu wa Serikali kwa kushirikana na Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Zanzibar, kufanya Sensa ya Watu na Makazi kila baada ya miaka kumi

Pili ni kukidhi matakwa ya Umoja wa Mataifa unaolekeza kila Nchi Mwanachama kupitia Ofisi za Takwimu kuhakikisha Sensa ya Watu ya Makazi inafanyika kila baada ya miaka mitano au kumi kutegemeana na Uchumi wa Nchi husika

Hivyo, nchi zote duniani ikiwemo Tanzania zinatekeleza Mpango Mkakati wa Umoja wa Mataifa wa Kufanya Sensa ya Watu na Makazi Duniani kwa Miaka ya 2020 ambao unatekelezwa kati ya mwaka 2015 hadi 2024

Utekelezaji wa Sensa, ni moja ya ahadi ya chama kama ilivyoainishwa kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020 Kifungu Namba 206 (i) ambacho kinaelekeza kufanyika Sensa na tafiti mbalimbali ikiwa ni pamoja na Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022

Aidha naye Mchumi wa Halmashauri ya Mji Tunduma Bwana Agustino Ngetwa aliwaelekeza washiriki juu ya faida kuu za Sensa ya watu na makazi kama ifuatavyo;

  • Ukusanyaji wa taarifa katika kipindi kimoja; ambapo hufanyika kila baada ya miaka 10 hivyo kuwa rahisi kulinganisha mienendo ya viashiria vya kijamii, kiuchumi, na kimazingira
  • Huwezesha kupatikana kwa viashiria vya kitakwimu hadi ngazi ya chini ya utawala
  • Matokeo ya Sensa hutumika kama takwimu za msingi kwa ajili ya kukokotoa makadirio ya idadi ya watu nchini
  • Hutumika kama rejea katika kutathmini na kuhakiki ubora wa matokeo ya tafiti mbalimbali
  • Taarifa za Sensa hutumika kama gawio la viashiria vya kila mwaka vinavyotumika kupima Malengo ya muda mfupi na Mrefu nchini, Malengo ya nchi za Kiafrica 2063 na Malengo Endelevu ya Dunia (SDGs 2030).


Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA May 24, 2022
  • TAARIFA KWA UMMA July 25, 2021
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA TUNDUMA May 03, 2022
  • KUITWA KAZINI June 25, 2021
  • Onyesha Zote

Habari mpya

  • TUNDUMA KINARA HOJA ZA CAG MKOA WA SONGWE YAPATA HATI INAYORIDHISHA MIAKA SITA MFULULIZO

    June 24, 2022
  • NMB TUNDUMA YAFUNGA MWAKA KIVINGINE

    June 20, 2022
  • NIMEFURAHISHWA SANA MAPOKEZI YA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO TUNDUMA

    June 22, 2022
  • KILA MTUMISHI AHAKIKISHE ANAFUNGA MWAKA AKIWA AMEMALIZA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAKE_TD MAGESA

    June 17, 2022
  • Onyesha Zote

Maktaba ya video

Ubunifu mkoa wa Songwe
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Songwe Shindani Blogspot
  • Watumishi Portal
  • Tunduma yapata hati Inayoridhisha
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2019
  • Tangazo la kazi sekta ya Afya
  • Sherehe za Muungano
  • Kibali cha Matangazo

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya Serikali

Idadi ya watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Msampania, Chapwa - Tunduma

    Sanduku la Posta: P. O. BOX 73

    Simu ya Mezani: +255 25 2957388

    Simu ya Mkononi: +255 752 807 767

    Barua Pepe: td@tundumatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya mji Tunduma. Haki zote zimehifadhiwa