• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
TUNDUMA TOWN COUNCIL
TUNDUMA TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MJI TUNDUMA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mipango
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu
      • Divisheni ya Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Divisheni ya Miundombinu na Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Udhibiti Taka na Usafi wa Mazingira
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
  • Fursa na Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya , Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Lishe bora kwa Afya imara
      • Mapambano dhidi ya Malaria
      • Mapambano dhidi ya Dawa za Kulevya
      • Mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI
    • Huduma ya Elimu
      • Huduma ya Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Huduma ya Elimu ya Sekondari
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya Kilimo
    • Huduma ya Mifugo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Maendeleo ya Jamii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Uchumi, Mipango Takwimu
      • Kamati ya Elimu, Afya na maji
      • Kamati ya Kazi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Ethics Committee
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Instagram
    • Facebook
  • Nyaraka
    • Nyaraka
    • Miongozo

MADARASA YAMEJENGWA KWA UBORA WA HALI YA JUU YANAKIWANGO CHA KIMATAIFA _RC KINDAMBA

Imewekwa : December 31st, 2022

Mkuu wa Mkoa kwa Songwe Mhe. Waziri Waziri Kindamba leo Disemba 31, 2021 amepokea madarasa katika Wilaya ya Momba kwa niaba ya Mkoa wa Songwe

Akiongea katika Hafla hiyo Mhe. Kindamba amesema ameridhishwa sana na ujenzi wa madarasa ndani ya mkoa wake na hususani hapa Halmashauri ya Mji Tunduma alipokuja kufanya uzinduzi ya kuyapokea madarasa kimkoa

“Nawapongeza sana Halmashauri ya Mji Tunduma kwa kweli mmeitendea haki Pochi ya mama Samia, Nimeridhika sana na ujenzi wa madarasa yote 12 tena ninyi mmejiongeza zaidi mmejenga na ofisi hongereni sana” alisisitiza Mhe. Kindamba

Wakati akikagua vyumba vya madarasa hayo 12 Mhe. Kindamba ameeleza kuwa Madarasa yana Malumalu, madirisha ya Aluminum, Dari za kisasa (Gypsum board), miundombinu ya Umeme, na Madawati 50 kila darasa ni hatua nzuri sana na ndio maana anayaita ni madarasa ya kimataifa

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Songwe amewaalika wazazi kuwa ifikapo Januari 09, 2023 wanafunzi wote wanatakiwa kuanza masomo hivyo kila mzazi ahakikishe kuwa mwanafunzi anaripoti shule bila kikwazo

“Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayongozwa na  Rais Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan imetoa fedha na kujenga madarasa pamoja ununuzi wa madawati bila kusahau vifaa vya kufundishia na kijufunzia hivyo hatuna upungufu wa kitu chochote ndani ya Mkoa wa Songwe kinachoweza kusababisha wanafunzi wasianze masomo, ni jukumu la kila mzazi kuhakikisha mtoto wake anaanza masomo mara moja” alisisitiza Mhe. Kindamba

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Momba Mhe. Fack Lulandala alimuelekeza Mkuu wa Mkoa wa Songwe kuwa Wilaya ya Momba ina Halmashauri Mbili yaani Halmashauri ya Wilaya ya Momba na Halmashauri ya Mji Tunduma ambapo Momba ilikuwa na ujenzi wa Madarasa 16 na Tunduma ilikuwa na ujenzi wa Madarasa 12, madarasa yote 28 yamekamilika na Wilaya ya Momba haina upungufu wa Madarasa kwa sasa

“Momba tunamshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia fedha za ujenzi wa madarasa kwa ajili ya kidato cha kwanza na tumetekeleza kwa kiwango cha kimataifa. Tunamumbea kwa Mwenyezi Mungu aendelee kumjalia Afya njema ili azidi KUUPIGA MWINGI” Alisema Mhe. Lulandala

Pia Mhe. Lulandala amekemea wazazi wanao waficha Watoto kuanza shule kwa sababu zozote zile waache kwani sheria itauchukua mkondo wake

“Rai yangu kwa wazazi wanaokwamisha Watoto kuanza masomo kwa sababu ya kuwaachia Watoto majumbani au kuwatumikisha kwa namna yoyote ile nasema hatua kali zitachukuliwa dhidi ya mzazi yoyote yule bila kujali wadhifa au cheo alichonacho” alisema Mhe. Lulandala

Kwa upande wake Mkuu wa Divisheni ya Elimu Sekondari Bi. Patricia Mbigili amesema kuwa Halmashauri ya Mji Tunduma sasa inakua kwa kasi kutokana na kuwepo kwa shule nzuri zinazoendela kujengwa

“Madarasa haya 12 tunayokabidhi leo yatasaidia wanafunzi ambao wameongezeka kwa asilimia kubwa kutokana na kuwepo kwa elimu Bure, pia kutonaka na Ubora na uzuri wa madarasa wanafunzi wengi tunategemea wataacha utoro kwani mazingira haya ni mazuri kwa kujufunza na kufundishia. Hivyo Ubora wa elimu hasa kwa Tunduma Mji utapanda zaidi” alisisitiza Bi. Patricia

 

Matangazo

  • Tangazo la Mkutano wa Kawaida wa Baraza la Madiwani kwa Kipindi cha Robo ya Tatu ya Mwaka wa Fedha 2024/2025 May 14, 2025
  • Orodha ya Majimbo Mapya na Yaliyobadilishwa Majina May 12, 2025
  • Taarifa kwa Umma Kuhusu Watahiniwa 694 Kufanya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita 2025 May 03, 2025
  • Taarifa kwa Umma February 27, 2025
  • Onyesha Zote

Habari mpya

  • Mashindano ya UMISSETA Ngazi ya Halmashauri Yaanza Rasmi

    June 02, 2025
  • DAS Nkinda: Ziara ya Viongozi DR Congo Ina Manufaa Tunduma, Taifa

    May 30, 2025
  • Tunduma TC Yang'ara Mpira wa Miguu, Kwaya, Bongo Fleva UMITASHUMTA

    June 28, 2025
  • Dkt. Kasululu Ahitimisha Mashindano ya UMITASHUMTA

    May 28, 2025
  • Onyesha Zote

Maktaba ya video

Ubunifu mkoa wa Songwe
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Songwe Shindani Blogspot
  • Watumishi Portal
  • Tunduma yapata hati Inayoridhisha
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2019
  • Tangazo la kazi sekta ya Afya
  • Sherehe za Muungano
  • Kibali cha Matangazo

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti ya Mkoa wa Songwe
  • OR-TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Msampania, Chapwa - Tunduma

    Sanduku la Posta: P. O. BOX 73

    Simu ya Mezani: +255 25 2957388

    Simu ya Mkononi: +255 756 427 307

    Barua Pepe: td@tundumatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya mji Tunduma. Haki zote zimehifadhiwa