• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
TUNDUMA TOWN COUNCIL
TUNDUMA TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MJI TUNDUMA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mipango
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu
      • Divisheni ya Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Divisheni ya Miundombinu na Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Udhibiti Taka na Usafi wa Mazingira
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
  • Fursa na Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya , Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Lishe bora kwa Afya imara
      • Mapambano dhidi ya Malaria
      • Mapambano dhidi ya Dawa za Kulevya
      • Mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI
    • Huduma ya Elimu
      • Huduma ya Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Huduma ya Elimu ya Sekondari
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya Kilimo
    • Huduma ya Mifugo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Maendeleo ya Jamii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Uchumi, Mipango Takwimu
      • Kamati ya Elimu, Afya na maji
      • Kamati ya Kazi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Ethics Committee
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Instagram
    • Facebook
  • Nyaraka
    • Nyaraka
    • Miongozo

TD Chaurembo Amshukuru Rais Samia kwa Maono Yake ya Kuboresha Huduma za Afya

Imewekwa : March 1st, 2025

Na Benton Nollo, Tunduma TC

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Tunduma, Mariam Chaurembo amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Sukuhu Hassan kwa dhamira yake ya dhati na maono ya kuboresha huduma za afya katika Halmashauri hiyo.

TD Chaurembo ameyasema hayo alipokuwa akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo kwa Halmashauri hiyo yamefanyika katika Hospitali ya Mji Tunduma tarehe 01 Machi 2025 ambapo Mgeni Rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Momba Mhe. Elias Mwandobo.

Chaurembo amesema wakati Wanawake wa Tunduma wanasherehekea siku hiyo muhimu, wanamshukuru sana Rais Samia kwa kujenga Hospitali mpya ya Mji wa Tunduma yenye miundombinu ya kisasa ambapo mpaka sasa zimeshatumika zaidi ya shilingi bilioni 6 katika ujenzi wa majengo pamoja na vifaa tiba na huduma zimeshaanza kutolewa.

Pia, Mkurugenzi Chaurembo amesema hivi karibuni Serikali imeleta fedha shilingi bilioni 2.3 kwa ajili ya ujenzi wa Jengo la ghorofa la Mama na Mtoto pamoja na Jengo la Upasuaji.

"Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Rais Samia, ameleta fedha ambazo zimejenga Vituo vya Afya Sita vipya ambavyo ni Chiwezi, Chapwa, Mpande, Chipaka, Tunduma TC na Mwakakati na vimeshakamilika kwa asilimia 99." Amesema Chaurembo na Kuongeza;

"Wanawake wa Tunduma sasa hivi hatutateseka tena kutembea umbali mrefu kufuata huduma za afya...maana kati ya Vituo hivyo tayari Kituo cha Afya Chipaka, Kituo cha Chiwezi vimeanza kutoa oparesheni ya Mama na Mtoto".

Pia, Chaurembo amesema kwa mwaka wa fedha 2024/2025 Halmashauri ya Mji Tunduma imetoa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 4.6 inayotokana na Asilimia Kumi (10%) ya mapato ya ndani ya Halmashauri kwa vikundi wa Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu.

Kadhalika, Chaurembo amempongeza na kumshukuru Rais Samia kwa kujenga Shule mpya ya Sekondari ya Wasichana ya Dkt. Samia SH ambayo mpaka sasa ujenzi wake mpaka sasa umegharimu shilingi bilioni 6.1.

Siku ya Wanawake Duniani husherehekewa kila mwaka tarehe 08 Machi ambapo kwa Mkoa wa Songwe kwa mwaka huu (2025) maadhimisho hayo yatafanyika wilayani Songwe.

Matukio katika Picha:

(Picha Benton Nollo na Julius Evandino, TTC).

Matangazo

  • Tangazo la Mkutano wa Kawaida wa Baraza la Madiwani kwa Kipindi cha Robo ya Tatu ya Mwaka wa Fedha 2024/2025 May 14, 2025
  • Orodha ya Majimbo Mapya na Yaliyobadilishwa Majina May 12, 2025
  • Taarifa kwa Umma Kuhusu Watahiniwa 694 Kufanya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita 2025 May 03, 2025
  • Taarifa kwa Umma February 27, 2025
  • Onyesha Zote

Habari mpya

  • Maonesho ya Fani za Ndani Yafana

    May 26, 2025
  • Mashindano ya UMITASHUMTA Mkoa wa Songwe Rarindima

    May 26, 2025
  • Madaktari Bingwa wa Dkt. Samia Wawasili Tunduma

    May 26, 2025
  • 'Hii Tunashinda kwa Kishindo'

    May 25, 2025
  • Onyesha Zote

Maktaba ya video

Ubunifu mkoa wa Songwe
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Songwe Shindani Blogspot
  • Watumishi Portal
  • Tunduma yapata hati Inayoridhisha
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2019
  • Tangazo la kazi sekta ya Afya
  • Sherehe za Muungano
  • Kibali cha Matangazo

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti ya Mkoa wa Songwe
  • OR-TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Msampania, Chapwa - Tunduma

    Sanduku la Posta: P. O. BOX 73

    Simu ya Mezani: +255 25 2957388

    Simu ya Mkononi: +255 756 427 307

    Barua Pepe: td@tundumatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya mji Tunduma. Haki zote zimehifadhiwa