• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
TUNDUMA TOWN COUNCIL
TUNDUMA TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MJI TUNDUMA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mipango
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu
      • Divisheni ya Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Divisheni ya Miundombinu na Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Udhibiti Taka na Usafi wa Mazingira
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
  • Fursa na Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya , Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Lishe bora kwa Afya imara
      • Mapambano dhidi ya Malaria
      • Mapambano dhidi ya Dawa za Kulevya
      • Mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI
    • Huduma ya Elimu
      • Huduma ya Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Huduma ya Elimu ya Sekondari
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya Kilimo
    • Huduma ya Mifugo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Maendeleo ya Jamii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Uchumi, Mipango Takwimu
      • Kamati ya Elimu, Afya na maji
      • Kamati ya Kazi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Ethics Committee
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Instagram
    • Facebook
  • Nyaraka
    • Nyaraka
    • Miongozo

MRADI WA UJENZI WA JENGO LA UTAWALA, MABWENI MAWILI NA MATUNDU NANE (08) YA VYOO KATIKA SHULE YA SEKONDARI MPEMBA

Start Date: 2018-02-01
End Date: 2019-04-16

UTANGULIZI

Shule ya Sekondari Mpemba ilianzishwa mwaka 2006 kwa usajili wa namba S.2303 na ni moja kati ya shule tisa (09) za Serikali katika Halmashauri ya Mji  Tunduma. Shule ina jumla ya wanafunzi 707, kati yao wanafunzi 663 ni kidato cha I hadi kidato cha IV ambapo wavulana ni 374 na wasichana ni 289, na kidato cha V ni wasichana 44 pekee. Shule ina jumla ya walimu 33, kati yao wanaume ni 15 na wanawake ni 18.

UTEKELEZAJI WA MRADI

Shule kupitia kamati mbalilmali za ujenzi ziliyoundwa na wananchi kutoka katika kila mtaa ndani ya kata ilianza kutekeleza ujenzi wa mradi huu mwezi Februari mwaka 2018 na mpaka sasa mradi huu umekamilika kwa asilimia miamoja. Miundo mbinu hii ilielekezwa kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha Tano ambao kwa Mwaka huu wa masomo waamesharipoti wanafunzi 44 na wanaendelea na masomo yao.Wanafunzi hawa ni wa michepuo ya sanaa yaani HGL na HKL.

UJENZI WA JENGO LA UTAWALA

Jengo hili limekamilika na linatumika. Limetumia jumla ya shilingi 76,247,964. Katika fedha hizi, shilingi 16,247,964 ni fedha kutoka katika mapato ya ndani ya Halmashauri na shilingi 60,000,000 ni fedha toka Serikali Kuu (P4R). Jengo hili lina jumla ya vyumba 09  na vyoo vitano kwa ajili ya walimu.

UJENZI WA MABWENI MAWILI YA WANAFUNZI

Mabweni mawili yamekamilika ambapo kila bweni lilitengewa kiasi cha shilingi 75,000,000. Hivyo mabweni yote mawili yalitengewa shilingi milioni 150,000,000. Mabweni haya yana jumla ya vyumba ishirini kila moja na kila chumba kina uwezo wa kubeba wanafunzi wanne (04) hivyo kila bweni lina uwezo wa kubeba wanafunzi 80.Vilevile mabweni haya yana vyoo vitano na mabafu matano kila moja na sehemu maalumu ya kufulia (laundry).

 

UJENZI WA BWENI NAMBA 01

Bweni hili limeshakamilika na linatumiwa na wanafunzi wa kidato cha tano walioripoti mwezi Julai, 2019. Ujenzi wa bweni hili umegharimu shilingi 101,303,000 kati ya fedha hizi, sh 75,000,000 ni fedha toka Serikalini Kuu (P4R) na sh 26,303,000 ni fedha kutoka mapato ya ndani ya Halmashauri.

UJENZI WA BWENI NAMBA 02

Bweni hili limekamilika na limegharimu sh 101,303,000 kati ya fedha hizi, sh 75,000,000 ni kutoka Serikali Kuu (P4R) na sh 26,303,000 ni fedha kutoka mapato ya ndani ya Halmashauri.

UJENZI WA MATUNDU 8 YA VYOO VYA WANAFUNZI

Ujenzi wa matundu ya vyoo umekamilika ambapo matundu 08 ya vyoo badala ya matundu 05 kama mradi ulivyoelekeza yamejengwa,  pia chumba kimoja maalumu kwa ajili ya watoto wa kike kimejengwa. Ujenzi huu umegharimu shilingi 7,846,036, kati ya fedha hizi, shilingi 5,500,000 ni fedha kutoka Serikali Kuu (P4R), na shilingi 2,346,036 ni mapato ya ndani ya Halmashauri.

LENGO LA MRADI NA MANUFAA YAKE

Lengo la mradi huu ni kupanua wigo wa utoaji elimu katika jamii ya wananchi wa Tunduma, Mkoa wa Songwe na Tanzania kwa ujumla kwa kuboresha mazingira ya utoaji wa elimu kwa watoto wa kike wanaofaulu, ili waweze kujiunga na kidato cha Tano (form v) katika Shule za Serikali. Hivyo wanufaika wa mradi huu ni wanajamii wote wa Mji wa Tunduma, Mkoa wa Songwe na Taifa kwa ujumla kwasababu wanafunzi waliojiunga kidato cha tano kwa Mwaka huu wa masomo wametoka maeneo tofauti tofauti ya nchi yetu ya Tanzania.

USHIRIKI WA NGUVU ZA WANANCHI

Mradi huu umefanikiwa kushirikisha nguvu za wananchi wa Kata ya Mpemba katika kazi zifuatazo;

(a)Kuchimba msingi wa majengo yote wakati wa kuanza kwa mradi huu

(b)Kuchimba mashimo yote makubwa na madogo ya vyoo

(c)Kuchota maji ya kujengea kila siku tangu ujenzi ulipoanza hadi ulipokamilika.

Kazi zote hizi zimegharimu kiasi cha sh 10,000,000

 

MAPATO YA NDANI YA HALMASHAURI

Halmashauri ya Mji wa Tunduma kupitia mapato yake ya ndani, iliwezesha ujenzi huu kukamilika kwa kuongeza kiasi cha shilingi milioni 101,200,000.

  • Shilingi 20,000,000 zilitumika katika utengenezaji wa vitanda 160 vya chuma (double daker) kwa ajili ya wanafunzi.
  • Shilingi 10,000,000 ziitumika katika kutegeneza mfumo wa maji kwa uchimbaji wa kisima kirefu, uwekaji wa mfumo maji mabwenini, ununuzi wa mota na pampu yake na tanki la maji. Kwa sasa kisima tayari kimeanza kutumika na maji yapo ya kutosha.
  • Shilingi ml 71,200,000 zilitumika kwa ajili ya ukamilishaji wa ujenzi wa jengo la utawala, mabweni mawili na matundu 08 ya vyoo kama mchanganuo wa matumizi yake ulivyoelekezwa katika utekelezaji wa kila mradi.

HITIMISHO

Tunaishukuru sana Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Mheshimiwa Rais John Joseph Pombe Magufuli kwa kutupatia mradi huu mkubwa sana katika shule ya Sekondari mpemba, Kata ya Mpemba, Vilevile tunaishukuru Halmashauri ya Mji Tunduma  kupitia Mkurugenzi wake kwa kutupatia fedha za kukamilisha mradi huu na kwa ushirikiano mkubwa waliotuonyesha tangu mradi ulipoanza hadi ulipokwisha. Mwisho tunawashukuru wananchi wa Kata ya Mpemba kwa ushiriki wao wa hali na mali katika kazi zote walizozifanya. Tunaahidi kufanya vizuri ili kiutangaza shule ya sekondari Mpemba  na Halmashauri yetu kwa ujumla.


Matangazo

  • Tangazo la Mkutano wa Kawaida wa Baraza la Madiwani kwa Kipindi cha Robo ya Tatu ya Mwaka wa Fedha 2024/2025 May 14, 2025
  • Orodha ya Majimbo Mapya na Yaliyobadilishwa Majina May 12, 2025
  • Taarifa kwa Umma Kuhusu Watahiniwa 694 Kufanya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita 2025 May 03, 2025
  • Taarifa kwa Umma February 27, 2025
  • Onyesha Zote

Habari mpya

  • Mashindano ya UMISSETA Ngazi ya Halmashauri Yaanza Rasmi

    June 02, 2025
  • DAS Nkinda: Ziara ya Viongozi DR Congo Ina Manufaa Tunduma, Taifa

    May 30, 2025
  • Tunduma TC Yang'ara Mpira wa Miguu, Kwaya, Bongo Fleva UMITASHUMTA

    June 28, 2025
  • Dkt. Kasululu Ahitimisha Mashindano ya UMITASHUMTA

    May 28, 2025
  • Onyesha Zote

Maktaba ya video

Ubunifu mkoa wa Songwe
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Songwe Shindani Blogspot
  • Watumishi Portal
  • Tunduma yapata hati Inayoridhisha
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2019
  • Tangazo la kazi sekta ya Afya
  • Sherehe za Muungano
  • Kibali cha Matangazo

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti ya Mkoa wa Songwe
  • OR-TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Msampania, Chapwa - Tunduma

    Sanduku la Posta: P. O. BOX 73

    Simu ya Mezani: +255 25 2957388

    Simu ya Mkononi: +255 756 427 307

    Barua Pepe: td@tundumatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya mji Tunduma. Haki zote zimehifadhiwa