• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
TUNDUMA TOWN COUNCIL
TUNDUMA TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MJI TUNDUMA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mipango
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miipangofiji na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwaimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Fursa na Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Uchumi, Mipango Takwimu
      • Kamati ya Elimu, Afya na maji
      • Kamati ya Kazi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Ethics Committee
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

MRADI WA UJENZI WA MAEGESHO YA MAGARI MAKUBWA YANAYOVUKA MPAKA WA TANZANIA - ZAMBIA

Start Date: 2019-01-22
End Date: 2019-09-06

UTANGULIZI 

Halmashauri ya Mji Tunduma Katika kipindi cha Mwaka wa Fedha 2018/2019 ilitengewa fedha kwa ajili ya mradi wa Kimkakati yaani Maegesho ya Magari Makubwa yanayovuka mpaka wa Tanzania –Zambia.

 HISTORIA YA MRADI

Eneo hili la ujenzi wa Maegesho lina jumla ya ukubwa wa ekari 17 ambazo Halmashuri ilitwaa kutoka kwa wananchi kwa kuwalipa fidia ili kufanikisha Ujenzi wa Mradi huu pamoja na ujenzi wa ofisi nyingine za taasisi.

 LENGO LA MRADI

Lengo la Mradi huu ni kuiongezea Halmashauri mapato yake ya ndani ili kupunguza utegemezi kutoka Serikali kuu na hatimaye kujitegemea kabisa katika uendeshaji wake.

 GHARAMA ZA MRADI

Halmashauri ya Mji Tunduma ilitengewa fedha jumla ya shilingi 1,630,000,000.00 kutoka serikali kuu kwa mwaka wa fedha 2018/2019 kwa ajili ya ujenzi wa Maegesho ya Magari Makubwa yanayovuka Mpaka wa Tanzania-Zambia kama mradi wa Kimkakati. Pia katika mapato yake ya ndani ilitenga Shilingi 119,000,000 kwa ajili ya kulipa fidia ya kutwaa eneo la kujenga mradi huu kutoka kwa wananchi.

Hadi sasa kiasi cha fedha kilichopokelewa na Halmashauri kwa ajili ya kutekeleza mradi huu ni shilingi 375,528,516.67 sawa na asilimia 23 ya fedha yote ya mradi, na kuifanya Halmashauri kuingia mkataba na SUMA JKT NYANDA ZA JUU KUSINI wenye thamani ya shilingi 1,628,808,150.45 bila VAT kwa awamu hii ambayo inajumuisha ujenzi wa uzio, jengo la choo, vibanda viwili vya kukusanyia ushuru, ujenzi wa mifereji na sehemu ya kuegesha Magari (Rigid Pavement). Mradi huu awali ulikuwa wa kuegesha magari 45 hadi 75 tu kwa siku lakini baada ya kikao cha wataalam wa Halmashauri (CMT) kukaa tarehe 30/04/2019 kiliamua ufanyiwe mapitio mkataba kwa lengo la kuongeza ukubwa wa eneo ili liweze kuegesha magari mengi zaidi. Baada ya kikao hicho Timu ya wataalam ilifanya kazi ya mapitio (Re-Design) na kuongeza eneo la kuegesha magari kuanzia magari 105 kwa siku.

 Mradi mzima wa kujenga Maegesho ya Magari Makubwa yanayovuka Mpaka wa Tanzania-Zambia mpaka utapokamilika tunatarajia utagharimu zaidi ya shilingi bilioni nane (Tshs.8bil) ambao utajumuisha eneo la Maegesho (pavement) la kuegesha Magari zaidi ya 300, Mgahawa wa chakula (Reustaurant), Vyoo vya kulipia (Ablution blocks), uzio wa tofari (Fence), Nyumba za kupumzika madereva na Makondakta (Rest house).

Hata hivyo tayari ujenzi umeshaanza kutekelezwa na jumla ya shilingi 375,528,516.67 zimeshatumika kumlipa mkandarasi malipo ya awali (advance payment) na hati ya kwanza ya malipo (1st Cert).Aidha kiasi cha Shilingi 99,000,000.00 kutoka mapato ya ndani kimeshalipwa kwa wananchi kama fidia ya kutwaa eneo la ujenzi huu na kiasi kilichobakia cha Shilingi 20,000,000.00 kitalipwa robo hii ya kwanza ya mwaka wa fedha 2019/2020.

Aidha mkataba huu ulisainiwa tarehe 22/01/2019 na ulikuwa wa siku 180 hivyo ulitarajiwa kukamilka 22/07/2019. Baada ya hapo Mkandarasi akaomba ongezeko la muda wa siku 91 lakini kulingana na sababu alizotoa zikapelekea kupatiwa siku 45 tu na hivyo kutakiwa kukabidhi mradi ifikapo tarehe 6/09/2019.

 MANUFAA YA MRADI

Manufaa ya mradi huu wa Ujenzi wa Maegesho ya Magari Makubwa yanayovuka Mpaka wa Tanzania–Zambia (Truck’s Parking) ukikamilika tunatarajia utaiongezea Halmashauri mapato kwa kiasi cha Shilingi za kitanzania 191,625,000.00 kwa mwaka kwa magari 105. Na mradi mzima utakapokamilika kwa hatua zote tunatarajia utaiongezea Halmashauri Mapato kwa kiasi cha fedha za kitanzania shilingi 547,500,000.00 kwa mwaka kwa magari 232 na kuongeza ajira kwa vijana hususani katika sekta ya Usafi na Mazingira.

 KAZI ZILIZOFANYIKA

Katika utekelezaji wa mradi huu kwa awamu hii kazi ambazo zimeshatekelezwa mpaka sasa ambazo ni sawa na asilimia hamsini na tano (55%) ni pamoja na:-

  • Kusafisha eneo la kazi (site clearance).
  • Kutoa udongo wa juu (top soil removal).
  • Kushindilia baada ya kutoa udongo (compaction)
  • Kujaza kifusi (G15) na kushindiria
  • Kuanza kupanga mawe kwa ajili kuanza kumwaga zege
  • Ujenzi wa vibanda vya walinzi na choo upo kwenye usawa wa linta


HITIMISHO

  • Tunaishukuru serikali kwa kutuwezesha kupata fedha kwa ajili ya utekelezajiwa mradi huu wa Ujenzi wa Maegesho ya Magari Makubwa yanayovuka mpaka wa Tanzania-Zambia na tupo tayari kupokea maelekezo.
  • Aidha tunashukuru sana Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dr. John Pombe Magufuli kwa uongozi wake bora ambao umewezesha miradi kutekelezwa katika Halmashauri yetu. Hii ni ishara tosha kabisa ya utekelezaji wa Ilani ya Uchanguzi ya CCM ya Mwaka 2015 inatekelezwa kikamilifu. 


Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA May 24, 2022
  • TAARIFA KWA UMMA July 25, 2021
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA TUNDUMA May 03, 2022
  • KUITWA KAZINI June 25, 2021
  • Onyesha Zote

Habari mpya

  • TUNDUMA KINARA HOJA ZA CAG MKOA WA SONGWE YAPATA HATI INAYORIDHISHA MIAKA SITA MFULULIZO

    June 24, 2022
  • NMB TUNDUMA YAFUNGA MWAKA KIVINGINE

    June 20, 2022
  • NIMEFURAHISHWA SANA MAPOKEZI YA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO TUNDUMA

    June 22, 2022
  • KILA MTUMISHI AHAKIKISHE ANAFUNGA MWAKA AKIWA AMEMALIZA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAKE_TD MAGESA

    June 17, 2022
  • Onyesha Zote

Maktaba ya video

Ubunifu mkoa wa Songwe
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Songwe Shindani Blogspot
  • Watumishi Portal
  • Tunduma yapata hati Inayoridhisha
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2019
  • Tangazo la kazi sekta ya Afya
  • Sherehe za Muungano
  • Kibali cha Matangazo

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya Serikali

Idadi ya watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Msampania, Chapwa - Tunduma

    Sanduku la Posta: P. O. BOX 73

    Simu ya Mezani: +255 25 2957388

    Simu ya Mkononi: +255 752 807 767

    Barua Pepe: td@tundumatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya mji Tunduma. Haki zote zimehifadhiwa